webnovel

chapter 61

Mwanga hafifu wa kibatari unaotoka sebuleni unafanya waonane vizuri,chumba kikiwa kinajaaa sauti za mahaba na pumzi za haraka zinazotoka midomoni mwao.Miili yao ikipanda joto Kila kupitako sekunde,mikono ya Tulya inaenda na kushika nywele za Nzagamba akimkandamiza zaidi aendelee kunyonya maziwa yake.Raha anayopata hajawahi kuihisi hapo awali.Nzagamba anaachia ziwa na kwenda kuchukua nyingine na kulitia mdomoni mkono wake ukichezea linguine " ohh!" sauti nzito inamtoka baada ya Tulya kujisogeza na kufanya maungo yao ya Siri yanayowaka moto yakitamani kukutana na kuwafanya kuwa mwili Mmoja kukutana.Uvumilivu wa Nzagamba unakuwa mdogo anatamani kukata hicho kipisi Cha nguo ya Tulya na kudumbukia Moja kwa Moja kumaliza kiu yake, lakini anaacha kwa sababu hataki kupeleka mambo haraka, anataka kufurahia Kila sekunde anataka raha anayoipata idumu kwa mda mrefu aifurahie kwa moyo wote maana imekuwa ikimtesa kwa mda mrefu isitoshe aliyelala chini yake ni mtu anayemfanya kuwa chizi ndani na nje.

"Nzagamba!" anaita Tulya baada ya Nzagamba kumng'ata kidogo kwenye ziwa,sauti yake inamfanya Nzagamba kuanza kunyonya ziwa kwa haraka zaidi kama mtoto mwenye njaa ya siku nzima,ikiwa ni ukweli kwani Nzagamba amekuwa na njaa hii kwa siku nyingi kiasi kwamba anatamani kummeza mzima mzima na bado hata Shiba kwani anauhakika mwanamke huyu atakuwa ni njaa yake ya milele hata akila hawezi kushiba.

"shiiiii,acha nikuhudumie usiwe na haraka" Nzagamba anamwambia baada ya kuona Tulya anazidi kujisugua zaidi kupunguza muwasho unaomtesa katikati ya mapaja yake.Macho ya Nzagamba yanaenda usoni kwa Tulya anatabasamu baada ya kuona macho yake yana aibu.Tulya anang'ata mdomo wake kichwani akijitukana kwa kuwa na kiherehere mpaka kinaonyesha." Tunao usiku mzima kwa kazi hii,sitaki Raha hii iishe haraka,nataka tuchukue mda kufurahia kama hatutaipata tena,au unataka tumalize haraka?"

anamuuliza sauti yake ikitoka nzito na ya kukwaruza.Tulya anatikisa kichwa kukataa " nataka kusikia sauti yako Tulya"anaongea macho yake yakiwa yameganda kwenye macho yake makubwa.

" hapana" sauti ya Tulya unatoka ndogo kiasi kwamba haamini kama yake " mhhh" anamuitikia na kwenda kukamata tena lipsi za Tulya kwa busu lingine akifanya vifua vyao vikitane.Anatoa rubega yake na sasa vifua vyao kuwa nyama kwa nyama kitendo kinaongeza msisimko zaidi.

Sauti ya kishindo kikubwa ikitokea nje inawashtua na kuwafanya wote kuacha walichokuwa wakifanya na kusikiliza lakini Kuna kuwa kimya.

" nini hicho?" anauliza Nzagamba akihema "Amna kitu"

Tulya anamjibu akimshika shingo na kuanza kumbusu.baada ya kimya kifupi pasipo kusikia chochote Nzagamba nae anaanza kumbusu lakini anaacha tena baada ya kusikia sauti ya mtu akigugumia maumivu." mama?!"

" amelala" Tulya anamjibu akiendelea kumbusu.

" hapana,nimesikia sauti ya mama" anamjibu akitaka kunyanyuka lakini Tulya anamshika na kumrudisha kifuani kwake.

" mama afanye nini usiku huu nje?utakuwa umesikia vibaya" anamjibu akimpapasa kifua chake asitake kabisa anyanyuke.Wakiwa bado wanabishana wanasikia sauti nyingine ya maumivu kutoka nje.

" ni mama" anaongea Nzagamba akinyanyuka na kutengeneza rubega yake.

" narudi Sasa hivi" anamwambia akianza kuelekea nje.

Tulya anabaki pale kitandani sura akiwa ameikunja kama kapaliwa ugoro,anamsikia Nzagamba akifungua mlango wa nje na kutoka anapeleka mkono wake kifuani na kufunika maziwa yake kwa kiganja Cha mkono wake mwili ukimsisimka anapokumbuka namna Nzagamba alivyokuwa anayanyonya maziwa yake Tabasamu linakuja mdomoni kwake lakini linatoweka baada ya kusikia sauti ya Nzagamba nje.

" mama umepatwa na nini?" sauti inakuwa ya juu na yenye wasiwasi anatafuta kitambaa chake Cha kifuani pale kitandani maana hata hajui Nzagamba alikitupa wapi.Baada ya kutokufanikiwa anashuka na kwenda kuchukua kingine anafunga maziwa yake huku akiwa anatoka nje.

Nje anamuona Nzagamba akimbeba mama yake na kuelekea ndani kwake.

" kapatwa na nini?" anauliza akienda kusimama pale walipo." mgongo wangu" anagugumia Bibi sumbo." ameanguka,nisaidie kufungua mlango"

Tulya anakimbia anafungua mlango " jamani mama ulikuwa unafanya nini nje na giza hili?" anauliza Tulya akiwa na wasiwasi.

MUDA MCHACHE ULIOPITA

Bibi sumbo alikuwa anajiandaa kulala mara anasikia sauti za miguu ya watu wakitembea na mlango kufunguliwa na kufungwa kwa nguvu .

" wamerudi mapema?!" anaongea akishangaa kwani alijua watachelewa kurudi kutokana na ngoma za harusi isitoshe aliyeolewa ni ndugu yake Tulya.Analaza kichwa chake kitandani na kujitengeneza vizuri anafumba macho yake anayafumbua sekunde hiyohiyo baada ya kusikia mzozo wa Nzagamba na Tulya." wanagombana au?!" anajiuliza akiwaza ni nini kimetokea huko kwenye sherehe.

Kutaka kujua anashuka kitandani na kusimama lakini miguu yake inakataa na kujikuta akijitupa kitandani tena na kukaa lakini sauti za ugomvi wa Nzagamba na Tulya zinamfanya sjikakamue na kuamka pale kitandani,anajisogeza ukutani na kushikilia anaanza kujisogeza kuelekea nje."Nzagamba kamfanya nini mschana wa watu?!" anajiuliza baada ya kufika sebuleni na kimsikia Tulya akiongea kama analia.

"ataelewa mda gani sijui kwamba ana bahati sana kumpata Tulya" anaendelea kuongea mwenyewe mpaka anafika na kufungua mlango wa nje lakini anakutana na kimya, zaidi anaona mwanga wa kibatari sebuleni unaooenya kwenye nyufa za nyumba na kutoka nje kuashiria ndani Kuna mwanga tofauti na nje kuliko na giza.

Anajiuliza kama alisikia vibaya kumbe ugomvi wa wanandoa ulishahamia chumbani walikopatana kwa njia tofauti.

Anataka kurudi ndani lakini anaona mbwa hawajafunguliwa anahisi Nzagamba kasahau kuwaachia ikiwa ni kweli kwani kwa mchezo aliouanzisha ndani hakuwa hata na wazo la mbwa nje.Anajikongoja mpaka nyuma ya nyumba na kuwafungulia mbwa,baada ya kumaliza anapiga hatua kidogo na kupunguza kibofu chake kilicho jaa.Anaanza kupiga hatua za taratibu kuelekea ndani kwa mbali akisikia sauti za ngoma na makelele ya vijana wanaokesha wakinywa na kufurahi kwenye sherehe." hizi ndio siku nzuri zaidi ukiwa bado mwepesi" anaongea sura yake ikijaa tabasamu kumbukumbu zake zikirudi nyuma siku za ujana wake.

" mhhh,kesho au kesho kutwa tutakuwa na mwezi mchanga ikiwezekana na mvua kidogo" anaongea akiangalia anga lililo jaa nyota tupu lakini Hali ya hewa ikiwa ni ya upepo mwembamba unaochoma kwenye ngozi na harufu nzuri ya mchanganyiko wa msimu wa miti iliyochipua pamoja na maua mbali mbali.Anapiga hatua lakini kutokana na kiza hakuona mti uliompiga mtama na kumpeleka chini.Hivyo ndivyo alivyoishia kuharibu mahaba ya watoto wake ndani.

Kwa Sasa Tulya na Nzagamba wanamwangalia kama kaumia sehemu nyingine yeyote na baada ya kusikia kilichomfanya aanguke hawajui wakasirike au vipi. mwishowe wanaaamua kujilaumu wao kwa kuongea kwa sauti ya juu la sivyo Bibi sumbo asingeumia na wao wangekuwa wanapata Raha ndani

" Tangu lini ikawa kazi yako kufungulia mbwa mama,usiku ukifika kwa nini usipumzike tu" anaongea Nzagamba sauti yake ikitoka Kali kidogo pasipo yeye kujua.

"najua" anaitikia Bibi sumbo akifunga macho yake" nendeni mkalale nitakuwa sawa" Nzagamba anatoka akifuatiwa na Tulya.

" usiku mwema" Tulya anamwambia huku akivuta pumzi ndefu na kutoa Nzagamba anamwangalia asimuelewe

" ina bidi nilale hapa,mama kaumia akihitaji kitu usiku itakuwaje?" isingekuwa Bibi sumbo ni mama mkwe wake angemmeza kwa kumharibia usiku wake lakini afanyeje inabidi awe mstaarabu.Nzagamba anamwangalia na kutoka Tulya anafunga mlango na kurudi chumbani.

" Haina haja ya kulala hapa mwanangu nitakuwa sawa" anaongea Bibi sumbo kwani aliwasikia mazungumzo Yao." usijali we lala,unadhani tukikala huko huku tunajua unaumwa na tumekuacha peke yako tutakuwa na amani?" anauliza Tulya akipanda kitandani." naona nimekuwa Mzee msumbufu,ambaye siwapatii hata amani ya usiku wanangu"

" ndio" anaitikiwa Tulya moyoni mwake.

Nje Nzagamba anaangalia katikati ya miguu yake na kumuona Nzagamba mdogo aliyekataa kulala kabisa baada ya mihemko aliyoipata na alikuwa anategemea kupata tulizo lakini mama yake kamharibia na mke wake nae kaamua kukaa mbali .Leo ule usemi wa usiku mwaka ndio ataujua. Anaamua kwenda kujitupa kwenye kichanja pale nje apigwe na upepo labda Hali itakuwa nzuri kidogo kwani anajua akiingia ndani namna ile atafanya kitu Cha kipumbavu ambacho hajawahi Fanya maisha yake.

Anavuta pumzi ndefu baada ya kulala Chali pale kitandani macho yake yakienda angani kuangalia nyota anajaribu kutoa akili yake kwenye kitendo kilichotokea chumbani kwao na Tulya Ili mwili wake ukae sawa lakini inakuwa ni kazi ngumu kuliko anavyodhania. namna anavyopigana na hisia zake ndivyo matamanio ya mwili wake yanavyoongezeka kitendo kinachomfanya atamani kwenda ndani kwa mama yake amchukue mkewe aondoke nae ndani kwake kwenda kumaliza alichokianzisha.Pasipo kujua anajikuta akiwa amesimama karibu na mlango wa mama yake.