Cecy hakuweza kumbembeleza kwani alitambua kuwa kuna wakati kutoa machozi ni muhimu. Moyo wa mwanadamu hauna mdomo, hivyo unazungumza kupitia machozi. Huzuni, hasira na majuto huweka uzito moyoni. Ni vyema kulia ili kuondoa mzigo huo. Na ndicho kitu Leah alichokuwa akifanya.
"What a sad life.", Leah alijisemea kimoyomoyo, "Kumbe hichi ndo kifo changu? Can't believe I used to kiss his hands, unaware that one day the same hands will kill me.",
Labda asingeenda kwenye ile sherehe mwaka 2009, maisha yake yasingekuwa yakikatishwa. Kijana yule mzuri, aliyevaa miwani kubwa na mwenye aibu leo hii alikuwa kaweka mikono yake shingoni akikamua maisha yake yatoke. Mwaka 2009 ndio chanzo.
Mwaka 2010 walisimama kanisani mbele ya familia zao na Mungu na kuapa kupendana na kuvumiliana kwenye shida na raha, hadi kifo kitakapowatenganisha. Nao wakafanywa mwili mmoja, familia moja.
Mlango wa chumba ulipigwa teke na Paul aliingia. Kwa mshituko mkubwa Leah aliangusha simu. Paul alikuwa kama faru litwetalo kwa hasira. Alianza kumsogelea Leah kama mwindaji;
"Bosi, ulipokuwa kwenye kikao, mimi ndio nilichukua simu yako na kumtumia message Cecy. Uliharibu mipango yake yote ulipoenda kukutana na Cecy gerezani, hivyo akaona amuue na akupakazie wewe kesi.",
Eris stood on a chair, dusting the top of the cabinet. Her phone rested on the table, Creep by Radiohead playing gracefully, cleansing her ears. It was her favorite song.